The Kingdom of Heaven

The Kingdom of Heaven MISSION - Preaching and teaching the good news of the Kingdom of Heaven.

06/04/2026

SAA YA KUJARIBIWA IKO TAYARI KUUJILIA ULIMWENGU WOTE ILI KUWAJARIBU WAKAAO JUU YA NCHI

“Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kujaribiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi” (Ufunuo 3:10).

Katika mstari wetu wa ufunguzi, Yesu mwenyewe amesema hapo, iko “saa ya kujaribiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.” K**a saa hiyo ipo na inakuja ya kujaribiwa kwa wakaao juu ya nchi, maana yake ni kwamba tunatakiwa kujiandaa kwa ajili ya kujaribiwa katika wakati huo.

Kusudi la kujaribiwa kwa watu wote ni ili kupima imani za watu k**a ni za kweli, na kuona k**a tunaweza kuvumilia mpaka mwisho pasipo kumkana Yesu na pasipo kutenda dhambi yeyote, na kusafishwa ili tuweze kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno lolote. Neno linasema;

“Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo BWANA aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki. Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza…..katika jangwa (wakati wa kujaribiwa), ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.

Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa k**a vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo. Nawe uzishike amri za BWANA, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha. Kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima; nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;

nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake yafukuka shaba. Nawe utakula ushibe, utamshukuru BWANA, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa. Jihadhari, usije ukamsahau BWANA, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo” (Kumbukumbu 8:1-11).

“Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha k**a fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu k**a dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu” (Zacharia 13:9).

“Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno” (Yakobo 1:2-4).

“Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi” (Warumi 5:3-5).

“Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu” (Waebrania 10:36-39).

“Wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi” (Matendo 14:22).

“K**a tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; K**a tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi; K**a sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe” (2 Timotheo 2:12-13).

“Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili” (1 Wakoritho 10:13).

“Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata k**a moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini k**a mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe. Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia. Maana mtu wa kwenu asiteswe k**a mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au k**a mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo. Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje? Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi? Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, k**a kwa Muumba mwaminifu” (1 Petro 4:12-19).

“Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka k**a dhahabu. Mguu wangu umeshik**ana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka. Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu” (Ayubu 23:10-12).

“Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu” (1 Petro 5:8-10). Amina!!

06/02/2026

UMUHIMU WA KANISA KUJIANDAA NA MATESO NA MAUAJI YANAYOKUJA ILI KUWEZA KUVUMILIA MPAKA MWISHO NA KUSHINDA

Paulo alisema, “Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu atateswa” (2 Timotheo 3:12).

Yesu alisema, “Angalieni, mimi nawatuma k**a kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara k**a nyoka, na kuwa watu wapole k**a hua. Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa. Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema. Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu. Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwafisha. Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka” (Mathayo 10:16-22).

Yesu pia alisema, “Wakati huo (wa siku za mwisho) watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu. Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana. Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka” (Mathayo 24:9-10,12-13).

Tena Yesu akasema, “Lakini, kabla hayo yote (ya vita) hayajatokea, watawak**ata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi, na kuwaua magerezani, mkipelekwa mbele ya wafalme na maliwali kwa ajili ya jina langu. Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu. Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza mtakavyojibu; kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga. Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu. Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu. Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu. Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu” (Luka 21:12-19).

“Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. K**a mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia. Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu.

Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka. K**a nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao. Yeye (awachukiaye ninyi) anichukiaye mimi (na) humchukia na Baba yangu. K**a nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa wametuona mimi (na ninyi) na Baba yangu, na kutuchukia. Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walituchukia bure” (Yohana 15:18-25).

Yesu akaendelea kusema, “Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili” (Ufunuo 2:10-11).

“Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile k**a wao” (Ufunuo 6:9-11).

“K**a tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu k**a utukufu ule utakaofunuliwa kwetu” (Warumi 8:17-18). Hii ndio faida ya kuvumilia mateso hayo yote katika siku hizi za mwisho. Mungu atusaidie sana wote katika kushinda hayo yote. Amina!!

05/25/2026

UMUHIMU WA KANISA KUJIANDAA KWA AJILI YA MAMBO YANAYOKUJA KATIKA SIKU HIZI ZA MWISHO

Yesu alikwisha kutuambia mapema juu ya yale yatakayokuwepo katika siku hizi za mwisho na kutuambia tujiandae kwa ajili ya hayo. Haya ndiyo Yesu aliyoyasema tuajiandae kwa ajili ya hayo; udanganyifu, vita, dhiki na mateso, kuchukiwa na mataifa yote, kuhubiri injili ya ufalme, kuokolewa katika kipindi hicho, na kuja kwake tena katika siku hizi za mwisho.

1. Udanganyifu

“Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi. Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi” (Mathayo 24:4-5,11).

“Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, k**a yamkini, hata walio wateule. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki. Kwa maana k**a vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu” (Mathayo 24:23-27).

2. Vita, njaa, matetemeko ya nchi, tauni, na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.

“Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali. Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu” (Mathayo 24:6-8).

“kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi; na njaa na tauni mahali mahali; na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni” (Luka 21:11).

3. Kusalitiwa, kupitia dhiki na mateso, na kuchukiwa na mataifa yote.

“Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu. Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana. Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka” (Mathayo 24:9-10,12-13).

“Na watakapowachukua ninyi, na kuwasaliti, msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni; kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu. Na ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, na baba atamsaliti mtoto, na watoto watashambulia wazazi wao, na kuwafisha. Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kusaburi hata mwisho, ndiye atakayeokoka” (Marko 13:11-13).

“Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu. Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu. Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu. Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu” (Luka 21:16-19).

“Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na k**a siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo” (Mathayo 24:21-22).

4. Kuhubiri Injili ya Ufalme, kuwa ushuhuda, kuwa waaminifu, na kukesha.

“Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja” (Mathayo 24:14).

“Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao. Na sharti Injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote” (Marko 13:9-10).

“Lakini, kabla hayo yote hayajatokea, watawak**ata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi, na kuwaua magerezani, mkipelekwa mbele ya wafalme na maliwali kwa ajili ya jina langu. Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu. Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza mtakavyojibu; kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga” (Luka 21:12-15).

“Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote. Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia; akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi; bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno” (Mathayo 24:45-51).

“Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo. Mfano wake ni k**a mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe. Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi; asije akawasili ghafula akawakuta mmelala. Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni” (Marko 13:33-37).

5. Kuokolewa katika kipindi cha dhiki kuu k**a Nuhu na familia yake walivyookolewa, na kuja kwa Yesu na wateule kukusanywa mbele zake

“Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake. Kwa maana k**a vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa kuwa k**a vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina, wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa. Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu. Lakini fahamuni neno hili; k**a mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja” (Mathayo 24:36-44).

“Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.

Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu. Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni” (Mathayo 24:29-33).

“Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, k**a mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima. Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu” (Luka 21:34-36).

05/18/2026

KANISA TUNAPASWA KUJIANDAA NA KUWA TAYARI KATIKA SIKU HIZI ZA MWISHO

Kanisa k**a Bibi-Arusi tunapaswa kujiandaa ili kukutana na Bwana-Arusi Yesu Kristo katika siku hizi za mwisho. Kanisa tunapaswa kujitayarisha katika Utakatifu (usafi wa kiroho), Maombi, Kukesha, Uaminifu, Uvumilivu, Upendo, Utayari wa kiroho, Kweli ya Neno, Kujitenga na ulimwengu, Maisha katika Roho, na Umoja katika Kristo.

1. Bibi-Arusi kujiweka tayari kwa ajili ya kukutana na Bwana-Arusi

Kanisa ni Bibi-arusi wa Kristo anayepaswa kujiweka tayari kwa ajili ya kukutana na Bwana arusi wake.

“Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari. Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu” (Ufunuo 19:7–8).

“Kristo naye alilipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote k**a hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.” (Waefeso 5:25–27).

“Kwa maana nimewaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi” (2 Wakorintho 11:2).

2. Kukesha na Kuwa Tayari

Yesu alilionya Kanisa mara nyingi kukesha kiroho na kuwa tayari wakati wote.

“Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu…Kwa hiyo ninyi nanyi iweni tayari…” (Mathayo 24:42–44).

Mathayo 25:1–13 inatufundisha juu ya kujiandaa kiroho na kuwa na mafuta katika taa zetu.

“Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara. Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.

Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi. Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie. Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi. Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa” (Mathayo 25:1-13).

“Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, k**a mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima. Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu” (Luka 21:34–36).

“Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo. Mfano wake ni k**a mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe. Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi; asije akawasili ghafula akawakuta mmelala. Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni” (Marko 13:33–37).

3. Utakatifu na Kujisafisha

Kanisa linajitayarisha kupitia utakatifu na kujitenga kwa ajili ya Mungu.

“Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu…..atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona k**a alivyo. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, k**a yeye alivyo mtakatifu. Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake. Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua.

Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, k**a yeye alivyo na haki; atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu” (1 Yohana 3:2–3).

“Fuataeni amani na watu wote, na huo utakatifu ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao” (Waebrania 12:14).

“Na tujisafishe na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukikamilisha utakatifu katika kumcha Mungu” (2 Wakorintho 7:1).

“K**a watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu; bali k**a yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu” (1 Petro 1:14–16).

4. Kuvumilia na Kudumu Katika Imani katika Siku za Mwisho

Kanisa limeitwa kuvumilia majaribu na kubaki waaminifu katika Imani.

“Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu. Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana. Kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. Lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokoka” (Mathayo 24:9-10,12–13).

“Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu” (Waebrania 10:35–39).

“Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho. Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia” (Yakobo 5:7–8).

“Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu” (Ufunuo 14:12).

5. Maombi na Maisha Katika Roho

Maandalizi katika siku za mwisho yanajumuisha maombi, kukesha kiroho, na kuishi katika Roho.

“Akaja akawakuta wamelala usingizi, akamwambia Petro, Je! Simoni, umelala? Hukuweza kukesha saa moja? Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu” (Marko 14:37-38).

“Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote” (Waefeso 6:18).

“Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele” (Yuda 1:20–21).

“Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini. Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru. K**a ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu. Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake” (Warumi 13:11–14).

“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho” (Wagalatia 5:16-17,25).

6. Kushik**ana na Kweli ya Neno la Mungu

Kanisa lazima libaki katika kweli ya Neno na kujiepusha na udanganyifu.

“Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi. Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, k**a yamkini, hata walio wateule. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki” (Mathayo 24:11,23-26).

“Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani” (1 Timotheo 4:1).

“Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao. Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao” (2 Timotheo 3:1–5,13-14).

“Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema” (Tito 2:11–14).

7. Kanisa Kujengwa Kuwa Makao Matakatifu ya Mungu

Maandalizi si ya mtu mmoja tu — mwili wote wa Kristo unajengwa pamoja kiroho.

“Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja. Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu. Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika Bwana. Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho” (Waefeso 2:19–22).

“Ninyi nanyi, k**a mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo” (1 Petro 2:5).

8. Kushinda na Kubaki Waaminifu na Wasafi hata mwisho

Yesu analiita Kanisa lake kushinda hadi mwisho.

“Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, k**a mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi” (Ufunuo 3:21).

“Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi. Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya” (Ufunuo 3:10–11).

“Tazama, naja k**a mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake” (Ufunuo 16:15).

Kanisa ni Bibi-arusi anayetakiwa kuwa tayari wakati wote, aliyejazwa Roho, aliyevikwa haki, anayekesha kwa ajili ya kuonekana kwa Bwana Yesu Kristo.

“Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa. Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu k**a kazi yake ilivyo. Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho. Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake” (Ufunuo 22:11-14).

“Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo!” (Ufunuo 22:17).

05/12/2026

JUST AS JESUS ​​WAS SENT BY THE FATHER INTO THE WORLD, IN THE SAME WAY IS JESUS ​​HAS ALSO SENT US INTO THE WORLD

“As you sent me into the world, so I have sent them into the world” (John 17:18).

Just as Jesus was sent by God the Father from heaven to give all people eternal life, the same way Jesus has also sent us from heaven to give all people eternal life. For Jesus said in the opening verse, “As you sent me into the world, so I have sent them into the world.”

Jesus said, “For this is the will of my Father, that everyone who looks to the Son and believes in him may have eternal life….” (John 6:40). He also said, “As you have given [your Son] authority over all flesh, that as many as you have given him may have eternal life. And this is eternal life, that they may know you, the only true God, and Jesus Christ whom you have sent” (John 17:2-3).

In the same way, Jesus has given us, the Church, authority over all nations so that we may give eternal life to all those whom he has given us. And eternal life, Jesus said, is this, that they may know the only true God, and Jesus Christ whom you have sent. Jesus was saying there that “eternal life” is God Himself. When people know God and Jesus whom he sent, they get eternal life.

Eternal life is God Himself, it is Jesus Himself. “And we know that the Son of God has come, and has given us an understanding, that we may know him who is true, and we are in him who is true, even in his Son Jesus Christ. This is the true God, and eternal life” (1 John 5:20). He says at the end there, Jesus is the true God, and eternal life.”

The God who is eternal life became flesh and that life was manifested in the world. “That which was from the beginning, which we have heard, which we have seen with our eyes, which we have looked at, and our hands have handled, concerning the Word of life; (and the life was manifested, and we have seen, and testify, and proclaim to you that eternal life, which was with the Father, and was manifested to us)” (1 John 1:1-2).

When all of us sinned, we lost God who is our life. And after losing God who is our life, we all died a spiritual death. “Therefore, just as sin entered the world through one man, and death through sin, and so death spread to all men because all sinned” (Acts 5:12). So all people in the world who do not have God (Jesus Christ) do not have life in them, they have death.

And when we believe in God in Christ Jesus, we are all given the right to eternal life again. “For if by the offense of the one man death reigned through the offense of the one, much more will those who receive the abundance of grace and of the gift of righteousness reign in life through the one, Jesus Christ. For as by one offense many were condemned to death, so by one act of righteousness many were justified to life. For as by one man’s disobedience many were made sinners, even so by one man’s obedience many were made righteous” (Acts 5:17-19).

“And this is the testimony, that God has given us eternal life; and this life is in his Son. He who has the Son has life; he who does not have the Son of God does not have life. I have written these things to you who believe in the name of the Son of God” (1 John 5:11-13).

When we help all people to know the true God and Jesus Christ, we are giving them eternal life and raising them from that spiritual death. So our brothers and sisters in Christ, let us continue to do this work that Jesus sent us to do to give eternal life to all people. Let us continue praying for all the people in the world who do not have Jesus Christ, so that God may help them to realize that they do not have life, they need to believe in Jesus to have life. God bless you. Amen!!

Address

Willmar, MN

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Kingdom of Heaven posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share