04/15/2024
ZAKA KATIKA AGANO JIPYA: BIBLIA INASEMAJE?
Bwana Yesu apewe,
Mmoja wa wanafunzi wa Kristo aliuliza swali juu ya zaka katika Agano Jipya. Nimepata msukumo kulijibu hili swali katika upana ili kumsaidia ye yote aliye na swali k**a hili.
ZAKA KABLA YA AGANO LA KALE: Kuna maeneo mawili ambapo tunaona zaka hata kabla ya Agano la Kale.
ZAKA YA IBRAHIMU KWA MELKIZEDEKI: Neno linatuambia kuwa baada ya Abramu kupata habari kuwa ndugu yake alitekwa na adui, Abramu alitumwa watumishi waendele kuwakomboa. Alipokutana na Melkizedeki, Abram alimpa fungu la kumi la vitu vyote (Mwanzo 14:20).
Zaka ambayo Abramu aliitoa kwa Melkizedeki ilikuwa hiari, na siyo k**a sheria kwani hapa hakukuwa na sheria. Mtu akiamua kutoa zaka k**a Abramu anaweza kufanya kwa hiari.
NADHIRI YA ZAKA YA YAKOBO: Yakobo aliota ndoto ambapo Mungu alimpa ahadi ambazo Mungu alimpa Ibrahimu na uzao wake. Ndipo Yakobo akaweka nadhiri kutoa zaka.
Mwanzo 28:20—2
20 Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae;
21 nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu.
22 Na jiwe nililolisimamisha k**a nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi.
Yakobo aliweka nadhiri ya kuwa Mungu akimbariki na kumpa mahitaji yake na kurudi kwa amani nyumbani kwa baba yake, ndipo atampa Mungu fungu la kumi.
Katika Agano Jipya, mtu anaweza kuweka nadhiri ya zaka k**a Yakobo kuwa Mungu akimtendea mambo fulani katika maisha yake atampa fungu la kumi.
K**a umeweka nadhiri ya kumtolea Mungu halafu usitoe, hapo itakuwa dhambi. Biblia inasema, bora usiweke nadhiri kuliko kuweka na kutokufanya (Kumbukumbu 23:21—22).
ZAKA KATIKA AGANO LA KALE
Katika Agano la Kale, kutoa zaka ilikuwa ni sheria (yaani ni lazima). Mungu aliagiza zaka ziendele katika maeneo makubwa matatu:
1. ZAKA YA MAONGEO KWA AJILI YA KULA MBELE ZA BWANA KILA MWAKA:
Zaka hii ilitolewa mara moja kwa mwaka. Zaka hii Mungu aliagiza mtoaji aile yeye na nyumba yake.
Kukumbuku 14:22—26
22 Usiache kutoa zaka ya kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.
23 Nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng’ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wako, daima.
24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako,;
25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako,
26 na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng’ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako.
Zaka hii watu walitoa ili wale mahali ambapo Mungu kaweka jina lake. Kusudi la zaka hii tunaliona mwisho wa msitari wa 23. Zaka hii ilikuwa mara moja kwa mwaka.
Katika Agano Jipya, hii zaka hatukuagizwa kwani hatuoni maeneo maalumu ambayo Mungu anayaweka jina lake. Jerusalemu pekee ndipo Biblia inasema Mungu ameweka jina lake milele (2 Nyakati 33:7).
Kwenye Agano Jipya hatuambiwi kwenda Jerusalemu kila mwaka kula zaka hii na familia zetu. Hii ilikuwa katika Agano la Kale.
2. ZAKA KWA MGENI, MJANE, YATIMA, NA MLAWI KILA BAADA YA MIAKA MITATU:
Kuna zaka ambayo Mungu alikusudia itolewe kwa mgeni, mjane, yatima, na kabila la walawi. Zaka hii ilikuwa inatolewa kila baada ya miaka mitatu.
Kumbukumbu 14: 27—29
27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe.
28 Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako.
29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi Pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale; na kushiba; ili kwamba Bwana, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
KWA WALAWI: Moja ya makusudi ya Mungu kuwapa kabila la Walawi zaka ni kwa sababu “wao hawakuwa na fungu wala urithi” (Hesabu 18:21—24). Katika Agano Jipya, zaka kwa ajili ya kabila la Walawi hatukuagizwa.
KWA MJANE NA YATIMA: Katika Agano Jipya, Mungu hakuweka sheria ya kutoa zaka kwa ajili ya mjane/yatima.
Katika Agano Jipya hatujaagizwa kutoa zaka kwa yatima, wageni, na wajane. Ila ni mapenzi kabisa hawa hatu katika jamii wasaidiwe kwa kadri mtu unavyoliwa. Hivyo mtu anaweza kutoa zaka au zaidi kwa hiari kwa ajili ya kuwasaidia wahitaji.
3. ZAKA KWA AJILI YA UKUHANI KWENYE HEKALU (ZAKA YA ZAKA).
Kuna zaka ambayo walawi walikuwa wanaitoa kwa kuhani mkuu. Kusudi la zaka hii ilikuwa kwa wale wanaofanya utumishi wa ukuhani katika nyumba ya Mungu.
Zaka hii inaitwa “zaka ya zaka” kwa sababu ni zaka iliyokuwa inatolewa katika zaka ambayo Walawi wameipokea.
Nehemia 10:38—39
38 Naye kuhani, mwana wa Haruni, atakuwako pamoja na Walawi, watwaapo zaka Walawi; nao Walawi wataipandisha [zaka na hiyo zaka] nyumbani mwa Mungu wetu, vyumbani, katika nyumba ya hazina.
39 Kwa kuwa wana wa Israeli na wana wa Lawi wataleta sadaka ya kuinuliwa ya nafaka, na mvinyo, na mafuta, vyumbani, kwa kuwa ndimo vilimo vyombo vya patakatifu, na makuhani watumikao, na mabawabu, na waimbaji; wala sisi tatutaiacha nyumba ya Mungu wetu.
Nimeweka msisitizo katika [zaka ya hiyo zaka] kwani hii ni zaka ambayo Walawi waliagizwa kuitoa kwa ajili ya utumishi katika hekalu Yerusalemu. Zaka hii ndiyo iliyotajwa katika Malaki 3:10 ambayo Walawi walikuwa wanaiba.
Malaki 3:8—10
8 Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mnebiibia zaka na dhabihu.
9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, [taifa hili lote.]
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue k**a sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwageni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
Mungu alisema kuwa makuhani Walawi na kabila yote ya Lawi wasiwe na urithi kwani Mungu ndiye urithi wao. Wao waliagizwa kula sadaka zinazotolewa (Kumbukumbu 18:1—2), hii ni pamoja na zaka k**a tumevyoona hapo juu.
Katika zaka ya Walawi, nao Walawi walitakiwa kutoa zaka katika zaka kwa kuhani mkuu kwa ajili ya watumishi katika nyumba ya Bwana, yaani [makuhani, mabawabu, na waimbaji].
Hivyo ukisoma context ya aina ya zaka ya Malaki 3:10 utaona kuwa hii ni zaka iliyotakiwa kutolewa na Walawi, yaani fungu la kumi la ile zaka ambayo wao wameipokea kwa watu.
Walawi walikuwa wanapokea zaka, lakini wao hawakuwa wanatoa “zaka ya hiyo zaka” kwa ajili ya watumishi watumikao katika nyumba ya Mungu. Ndio maana Mungu anasema walikuwa wanaiba.
Walikuwa wanaiba kwa sababu Walawi walipokea zaka, ila wao hawakuwa wanatoa. Ndio maana laana ilienda kwa taifa lote. Wale waliokuwa wanaiba walisababisha Mungu kulaani taifa lote la Israel.
Zaka ya zaka ndiyo ina baraka iliyotajwa katika Malaki 3:10b: “mjue k**a sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwageni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.”
ZAKA YA ZAKA KATIKA AGANO JIPYA: Zaka ya zaka iliyotajwa katika Nehemia 10:38 na Malaki 3:10 kanisa halikupewa hii sheria kuitoa kwani ule ukuhani wa Walawi hekaluni haupo. Hivyo baraka ya Malaki 3:10b siyo kwa ajili ya kanisa.
“Nyumba yangu” ambayo imetajwa katika Malaki 3:10 siyo “mahali wanapokutanika kuabudu” katika Agano Jipya. Mtu akitoa zaka kwa hiari kwa ajili watumishi wanaotumika kanisani haina shida, ila hii siyo sheria katika Agano Jipya.
ZAKA KATIKA AGANO JIPYA (YAANI BAADA YA KUFUFUKA KWA YESU)
Kwenye Agano Jipya, Mungu hakuweka utoaji zaka k**a sheria. Agano Jipya limesisitiza juu ya “kutoa kwa moyo,” yaani kwa kadri mtu unavyoamua ndani ya moyo wako. Kwenye Agano la Kale, kutoa zaka ilikuwa ni sheria, siyo hiari.
Na tunaona kuwa zaka ambayo Walawi wahakutoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu ndio ilileta laana. Zaka ya wajane/yatima, au ile ya kila mwaka siyo iliyoleta laana kwa taifa.
Mitume walipoagiza “mambo ya lazima” kwa watu wamataifa, kuishika torati haikuwa mojawapo na hii ilimpendeza Roho Mtakatifu, yaani ilimpendeza Mungu (Matendo 15).
Bwana Yesu alipokuwa anawahubiria wale waliokuwa chini ya torati, alizungumza na Mafarisayo alisemea:
“Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa Mungu; iliwapasa kuyafanya hayo kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili” (Luka 11:42). Pia soma Mathayo 23:23.
Bwana Yesu alisema kuwa Mafarisayo walikuwa “wapenda pesa” (Luka 16:14). Hivyo unaweza kuelewa kwa nini waliweka mkazo katika utoaji sadaka, ila mambo ya muhimu zaidi k**a upendo kwa Mungu, waliyaacha.
Bwana Yesu alikuwa anaongea na watu ambao wako chini ya sheria ya Musa na aliagiza watoe zaka, kutoa sadaka ya kutakaswa kwa aliyekuwa na ukoma (Marko 1:40—44), na sadaka za “madhabahuni” zilizopo katika torari (Mathayo 5:23—25).
Baada ya kufufuka kwa Yesu Kristo, yaani katika Agano Jipya, mitume hawakuagiza utoaji zaka, sadaka za kutakaswa, au sadaka zingine katika madhahabu hekaluni.
Katika Agano Jipya, sadaka ambayo Mungu ameiamuru ni kwa ajili ya wale ambao wanapeleka injili. Neno linasema, wanaopolekea injili wanastahili posho/ujira (Mathayo 10:10; Luka 10:7; 1 Timotheo 5:17—18). Mtume paulo pia aliandika, na kusema,
“Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekalu hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiayo madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale wauhubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili” (1 Wakorintho 9:13—14).
Hivyo ni amri ya Mungu kwa watu wake kutoa kwa ajili ya wale wanaopeleka injili. Kwa matajiri na wale ambao Mungu amewawezesha kipesa, neno linasema, kutoa na kushirikiana na wengine kwa moyo (1 Timotheo 6:8—9). Hii siyo amri.
Katika Agano Jipya, hakuna andiko ambalo linazungumza juu ya utoaji zaka k**a sheria. Mtu anaweza kutoa zaka kwa hiari na akapeleka anapoongozwa, ila siyo sheria.
Kila anayefundisha zaka k**a sheria kwa kanisa lazima atumie maandiko ya Agano la Kale tun a context ya Malaki 3:8—10 lazima ibadilishwe ili “nyumba ya Mungu” iwe “kanisa” na “makuhani Walawi” wawe watumishi kanisani. Hili siyo fundisho la mitume.
Ila kwa wale ambao Mungu amekujalia, ni mapenzi ya Mungu 100% kutoa kwa moyo. K**a ni kusaidia wenye shida, kutoa zaka ya hiari, kutoa kwa watumishi, yote haya yanampendeza Mungu yakifanywa kwa moyo safi.
Ila kutoa kwa wainjilisti kupeleka injili, hii siyo hiari, bali ni amri kutoka kwa Mungu.
Ubarikiwe,
Jacob Makaya